Samoszóst

Двухминутка медитации для любителей змеиного языка.
Во-первых, структуры вроде “вас тут не стояло.”
Przed drzwiami, na schodkach, siedziało dwóch typów w skórzanych kurtach i spiczastych futrzanych czapkach.
Во-вторых, изящные конструкции для “внесколькером”.

Jest nas sześciu. Miałem samoszóst na całą szajkę uderzyć, czy jak?
Zjechał z mogiły i samoczwart, z nieodstępnym Fiszerem, Biegańskim i Zarębą, odprawiwszy na stronę chorągiew wolonterów, ruszył pomiędzy walczące wojska.
Что у нас холодное и огнестрел, то у поляков broń biała и broń palna.

Макияж госбюджета

1) Французы ругаются на Руссеф за “макияж госбюджета”.
Le reproche officiellement fait à Dilma Rousseff est un maquillage des comptes publics.
2) Первый английский фразеологизм, который приходит в голову в этой связи – “to cook books”. Как, например:
Her opponents needed only a simple majority of the 81 members of the senate to force her to stand aside and go on trial for allegedly cooking the government’s books.
3) Русские в таких случаях говорят “причёсывать баланс”.

Русский латышский

Cittautieši, досконально знающие латышский, обнаруживают свою инаковость в занятных мелочах.
1. Они настойчиво не путают ka un kad, всегда скажут “jāizlasa grāmata”, долго не переходят на tūkstots.
2. Случайным образом расставляют узкие и широкие е, а некоторые даже не знают о том, что они разные. Точные правила распределения ведомы лишь Эндзелину, но латыши произносят слова как привыкли, и по странному совпадению то, как они их произносят, считается правильным 🙂
3. Не отдают себе отчёт, что о иногда “уо”, а иногда “о”. Например, joga un Olga, bet koks un lode.

清 голубая вода

Японский иероглиф 清 означает прозрачность, чистоту, невинность.
Он состоит из двух частей: 青 и 水 (голубая +вода).
Об этом мне рассказал Kiyoshi Takahashi, в чьё имя этот иероглиф входит.
Вторая часть имени Кийоши, иероглиф 志 – это комбинация знаков “сердце воина”, 心 + 士, которые вместе означают “решимость”.

Учебные тексты на суахили 4: Coca-Cola ilivyopata jina lake

Coca-Cola ni moja ya kampuni maarufu duniani, ambayo hutengenezwa soda maarufu ya Coke na vinywaji vingine vya soda. Lakini, ilikuwaje hadi ikawa na jina hilo?

Labda umewahi kusikia kwamba Coca-Cola wakati mmoja ilikuwa na kiungo cha kusisimua ambacho kiliwafanya wateja kulipenda sana. Hii ni moja ya vilivyochangia jina lake.
“Coca”, kwa Kiswahili koka, ni jina la jani la mmea wa koka, moja ya viungo ambavyo mvumbuzi wa kinywaji hicho, mwanakemia wa Atlanta John Stith Pemberton, alichanganya na shira kutengeneza kinywaji chake.
Majani ya koka hutumiwa kutengeneza kokeini.
Wakati huo, mwishoni mwa karne ya 19, ilikuwa kawaida kwa majani ya koka kuchanganywa na divai na kuwa kinywaji cha kuchangamsha mwili.
Kinywaji kipya alichotengeneza Pemberton kilikuwa njia nzuri ya kukwepa sheria zilizoharamisha uuzwaji wa pombe.
Sehemu hiyo nyingine ya jina Coca-Cola inatokana na kiungo kingine chenye nguvu, ingawa si maarufu sana.
Kiungo hiki ni kola.
Ganda ambalo huwa na kokwa za kola ndani yake huwa na urefu wa inchi mbili na kabla ya kukauka, huwa za rangi ya kijani.
Ndani yake huwa na sehemu yenye fundo za rangi nyekundu au nyeupe kabla hazijakauka.
Asili ya kola ni Afrika Magharibi na zimekuwa zikitafunwa kwa miaka mingi na wenyeji kama kitu cha kuchangamsha mwili.
Kokwa hicho huwa na kafeini na theobromine, ambavyo hupatikana pia kwenye chai, kahawa na kakao. Zina pia sukari na kolanin, ambayo huaminika kuwa kichangamsha moyo.
Kufikia karne ya 19, kola zilianza kusafirishwa Ulaya na Marekani na zikaanza kutumiwa katika tembe zilizokusudiwa kutumiwa kuongeza nguvu mwilini.
Muda si muda, zilianza kutumiwa kwenye vinywaji. Kinywaji kimoja maarufu kilikuwa Vin Mariani, cha Ufaransa kilichotayarishwa kwa kuchanganya maji ya coca na divai nyekundu.
Kilitengenezwa na mwanakemia Mfaransa Angelo Mariani, mwaka 1863, na Papa Leo XIII alikuwa mmoja wa waliokipenda sana.
Malkia Victoria wa Uingereza, Thomas Edison, na Arthur Conan Doyle pia walikipenda sana.
Pemberton, naye alijitokeza na mchanganyiko wake akifuata mtindo huu lakini yeye hakutumia divai bali alitumia shira.
Baada ya muda kokeini iliacha kutumiwa kwenye vinywaji, baada ya kutambuliwa kama dawa ya kulevya lakini kola ziliendelea kuwa maarufu.
Kwa sasa, viungo pamoja na utaratibu wa kutayarisha soda za Coca-Cola huwa siri kuu, lakini taarifa husema huwa kola hazitumiwi tena. Badala yake, kampuni hiyo hutumia kemikali kuunda ladha sawa na ya kola.
Hata hivyo, jina halijabadilika.
Inakadiriwa kwamba chupa 1.9 bilioni za Coke huuzwa kila siku.

BBC
http://www.bbc.com/swahili/habari-37544715

Учебные тексты на суахили 3: Maneno mapya

Maneno mengi yanatungwa kwa sababu mahsusi na hukubalika kutumiwa na watu polepole baada ya muda mrefu.

Kawaida ya lugha ni kwamba hukua. Kukua kwake ni kwa kuongezeka kwa maneno yaliyo mapya au kwa maneno yaliyopo kuwa na maana mpya. Inasemekana kwamba lugha ya Kiingereza, kwa mfano, kila mwaka huongezeka maneno mapya yapatayo 20,000.

Hivyo ni sawa na kusema kwamba kila siku maneno mapya 55 yanaingia katika lugha hiyo. Kwa hesabu nyingine ni kwamba kila saa, mchana na usiku, maneno mapya mawili au matatu yanabuniwa katika lugha ya Kiingereza.

Kuna wenye kusema kwamba idadi hiyo ya maneno mapya ni ya kutia chumvi. Wengine wanasema kwamba kwa hakika idadi hiyo ni ndogo kuliko ilivyo hasa. Miongoni mwa maneno hayo mapya ni yale yanayohusika na sayansi, teknolojia pamoja na ya kibiashara.

Ingawa Kiswahili kinakua hata hivyo haielekei kwamba lugha hii inakua kwa kiwango kama hicho cha kuongezeka idadi kubwa hivyo ya maneno mapya.

Maneno mengi yanatungwa kwa sababu mahsusi na hukubalika kutumiwa na watu polepole baada ya muda mrefu. Ni taabu kung’amua ni lini hasa neno jipya linapoanza kukubalika kutumiwa. Idhaa ya Kiswahili ya BBC yenyewe ilikuwa zamani katika mstari wa mbele miongoni mwa waliokuwa wakitunga maneno mepya ya kutumiwa katika Kiswahili. Maneno kama ‘katiba’ na ‘kutaifisha’, kwa mfano, yalianza kwanza kutumiwa na Idhaa ya Kiswahili ya BBC na polepole yakakubaliwa na kuanza kutumiwa na vyombo vingine vya habari vyinavyotumia lugha ya Kiswahili.

Neno ‘runinga’ lenye maana ya televisheni lilitungwa na Sheikh Ahmed Nabahany wa Kenya na sasa limekwishaanza kutumika na kukubalika.

Maneno mengine mepya katika lugha ya Kiswahili huanza kutumiwa na vijana barabarani mijini. Nchini Kenya, kwa mfano, baadhi ya maneno yanayotumiwa na vijana mitaani katika lugha yao ya ‘sheng’ huanza pia kutumiwa na wengine katika jamii na mwishowe hukubalika kuwa miongoni mwa msamiati halali wa Kiswahili.

Kwa hakika, katika miongo ya hivi karibuni lugha ya Kiswahili imekua sana kwa kuingizwa maneno mepya katika msamiati wake. Maneno hayo huwa ama yametungwa au yamebadilishwa kutoka lugha nyingine ili yalingane na Kiswahili au ‘yameazimwa’ kutoka lugha nyingine. Madhumuni ya maneno hayo mepya ni kuelezea dhana ambazo hazijakuwako katika ulimwengu wa Kiswahili.

Mengi ya maneno mepya yamebuniwa katika sayansi na teknolojia. Huo ni ushahidi ulio wazi kwamba Kiswahili bado hakijakomaa. Hata hivyo, juu ya kubuniwa maneno chungu nzima yaliyo mepya maneno hayo bado hayatumiwi na watu wa kawaida. Kama yanatumiwa basi hutumiwa na watu wachache tu walio wataalamu wa fani hizo.

Kuna maneno mengine ambayo hata hao wataalam hawayatumii kwani maneno hayo hubakia katika kumbukumbu za maktaba au za walioyabuni maneno hayo.

Dosari moja lililopo katika msamiati wa Kiswahili ni kwamba hata makamusi yanayosifika yanakosa baadhi ya maneno mepya (na hata ya kale) yanayotumiwa sana siku hizi na watu wa kawaida.

Katika miaka ya hivi karibuni kumetungwa makamusi kadhaa yenye kujaribu kukidhi haja ya kuyaeneza na kuyaeleza maneno mepya ya Kiswahili yanayohusika na mambo ya sayansi, tekinolojia na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Mifano mizuri ni Kamusi ya Awali ya Sayansi na Tekinolojia na Kamusi ya Kemia, Fizikia na Biolojia.

Kwa hakika, kila chumba cha habari kinahitajika kiwe na makamusi kama hayo yenye kuelezea maana ya maneno ya kisayansi na ya kiteknolojia.

Tangu mwisho wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia kumepatikana maendeleo makubwa duniani katika nyanja za sayansi, ufundi, viwanda, sayansi ya jamii na utamaduni pamoja na elimu. Maendeleo hayo makubwa yamezusha haja ya kubuni msamiati mpya wa maneno yatayotumika katika nyanja hizo si katika lugha ya Kiswahili tu bali pia katika lugha nyinginezo, pamoja na ya Kiingereza.

Hivi sasa kuna dhana kwamba ulimwengu mzima ni ‘kijiji kimoja’ tu chenye mifumo ya hali ya juu ya kisiasa na kiuchumi kutokana na mapinduzi makubwa yaliotokea katika nyanja za usafiri na mawasiliano. Hivyo, maneno mepya yanayotumiwa katika lugha za kigeni, hasa ya Kiingereza, ni rahisi sana kupenya na kuingia katika msamiati wa Kiswahili. Maneno hayo zaidi huwa ni ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

Ugumu wa kupata maneno ya Kiswahili yanayoweza kusibu kutumika katika nyanja hiyo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano umesababisha maneno ya Kiingereza yanayotumika katika nyanja hiyo yawe sasa yanatumika, bila ya kubadilishwa sana, katika lugha ya Kiswahili. Mifano iko mingi: folda (folder), kiibodi (keyboard), yuza nem (user name), kudelete (to delete), kusaaf au kubrauz (to surf, to browse), skrini (screen) na kontrol key (control key).

Jambo lililo muhimu ni kwamba tunapoanza kuyatumia maneno mepya yaliokubalika tuyatumie kwa njia ambayo itakuwa rahisi kwa msikilizaji au msomaji kuelewa unakusudia nini.

Maneno kama ‘tabia nchi’ na ‘utandawazi’ ingawa hayakuanza kutumika kwa muda mrefu sana hivi sasa yamekwishakuwa maneno ya kawaida yanayofahamika na wasikilizaji wa redio au televisheni au wasomaji wa magazeti na wa mablogi.

BBC Academy
http://www.bbc.co.uk/academy/swahili/language/new-words/article/art20131030124225972